PADRI KARUGENDO ACHA VIONJO!
Mwanafalsafa wa siku nyingi Permanides anatuasa juu ya ukweli anasema watu wanachanganya kati ya ukweli kadri unavyojitokeza kwao-relative truth na ukweli halisi-objective truth anasema ni vizuri kuangalia kitu kama kilivyo na si-vinginevyo,hii ilimfanya mwanafalsafa Plato kuugawa ulimwengu katika makundi mawili,yaani ulimwengu wa busara na akili-intelligible world na ulimwengu wa mwonekano-sensible world na kadiri ya Plato wale wenye busara na fikara sahii wapo kwenye ulimwengu wa ukweli na wale wenye vionjo wapo kwenye ulimwengu wa maoni/maono!
Hivyo katika kutoa hoja zetu ni vyema tufuate taratibu za fikara sahihi na si-vionjo kama Karugendo!
Makala aliyojibu Padri Privatus Karugendo ya jumapili 25,Febr 2007,ISSN 0856-9762 Na.814 katika gazeti hili la Tanzania Daima yenye kichwa cha habari “Sijapotoka ni maoni!” inaonyesha mambo makuu mawili mosi Karugendo bado hajaelewa kwa kina kuhusu kondomu,ukimwi,na sakramenti ya kitubio! Pili Karugendo anashindwa kutofautisha kati ya ukweli kadri unavyojitokeza kwake na ukweli ulivyo na hili ni tatizo la wengi!Binafsi sitachoka kumwelimwisha babu yangu na matumaini ya kumpata yapo!
Ukisoma kwa makini katika makala zile mwandishi “amejifunua” na binafsi nimepata faida ya kumjua ni nini anachowaza! Na ndio maana leo namwambia aache vionjo/maoni afuate ukweli ninaomweleza!
Simkatazi siku nyingine kutokuandika maoni yake la hasha! Unapoandika maoni ni sawa na mvuvi anayetupa ndoana mtoni! Maoni ni njia ya kuupata ukweli na unapopewa ukweli haraka uufuate, namwambia sasa afuate ukweli na awe muumini wa ukweli kondomu,kitubio,na ukimwi!
Mwandishi anasema amefanya kazi ya upadre kwa miaka 17 hivyo anaelewa anachozungumza na mimi kama mjukuu niache opium! Hii inanifanya nicheke kidogo! Hapa kuna maswali najiuliza kwa kuwa karugendo amefanya kazi ya upadri kwa miaka 17 na kwa mujibu wa mafundisho tunaambiwa mapadri huishi useja,je yeye karugendo alifuata maadili? Na kama Alifuata kwa nini anasema watu hawawezi kuacha ngono kabla ya ndoa? Na kama hakufuata je anafikiri sababu ya yeye kushindwa kuuishi useja wake ni sawa kwa watu wote? Ni sababu zipi zilizomfanya ashindwe? Je alitumia kitubio na akashindwa kujizuia?
Pia naona mwandishi amepotoshwa na methali ya kiswahili isemayo “Asiyesikia la mkuu huvunjika guu” napenda aelewe kwamba ni kweli mimi ni mjukuu wake kiumri! Si kiuelewa wa mada hii! Hivyo methali yake haina uhusiano kabisa.
Asiyesikia la mkuu huvunjia guu maana yake ni kwamba asiye sikiliza la msema kweli juu ya jambo fulani ilhali yeye ama hajui au ana elimu ndogo basi mtu huyo ni rahisi sana kupata madhara kwa baadaye! Karugendo kwa vile amesema anatoa maoni basi yeye ndiye mjukuu kwa maana ya uelewa wa suala hili hata kama ameandika kuhusu ukimwi tangu 1997 hilo halijalishi! Pili akumbuke kuwa “ukubwa wa pua si-wingi wa kamasi”
Mwandishi anasema hata Yesu akija leo hii atakaa na wanaotetea kondomu kwani alikaa na mafarisayo,malaya na wengineo! Kwa kuwa Yesu ni mwalimu wa wanaoitafuta kweli ni kweli kabisa atakaa na wote anaowataja mwandishi!
Kisha Yesu atawauliza Ninyi ni akina nani? Ni nini shida yenu hasa mpaka mkatengeneza kondomu? Kwa nini hamjafikiria juu ya kuwafundisha watu kuacha kufanya ngono? Mnajua kama ninyi ndio ma-CEO/GMs wa hapa duniani? Kwa nini mnaitia dhambi manukato? Mbona mnakana cheo chenu na mnajiita wajasiriamali wa kondomu? Kama mmeshindwa je mmemuuliza Baba yenu aliye mbinguni? Amesemaje?
Yesu akiwa anawauliza maswali haya wataangaliana wao kwa wao na kuanza kunyoosheana vidole! Yesu atawaambiwa yaliwapasa muwe na akili ya uchaji si ya kibinadamu! Nendeni mkatengeneze bustani na kurudisha heshima ya tendo la ndoa duniani! Mkifanya hivyo baba yenu atawasamehe na mtatimiliza azma yake katika ulimwengu huu! Kisha yesu atawatoka!
Karugendo ameshindwa kutofautisha kati ya dhambi na mtenda dhambi! Kwa kadiri ya mafundisho yatupasa kutowachukia watenda dhambi ila dhambi! Na Yesu anaongea na wote hususani wenye dhambi,hawezi kukataa kukaa na kuwaelimisha watenda dhambi!(kwa maana nyingine Yesu hawezi kuitetea dhambi!)
Na ni kweli kwamba sisi sote ni watoto wa Mungu na wajasiriamali wa kondomu nao wataitwa watoto wa mungu lakini kuna tofauti kubwa sana kati ya watoto wa mungu na watoto wanaomtii Mungu!
Kuitwa mtoto wa mungu ni “offer” ukikubali na kumtii mungu ni “contract” na utaitwa mtoto mtiifu wa mungu Kwa hiyo watengenezaji na wapiga debe wa kondomu kama karugendo kazi kwao ama waikubali(accept) au waikatae(reject).Offer hii ipo muda wote kadri wao watakavyoishi ila wakumbuke kuwa “Killing time is not murder its suicide” soma (Yn 12:23-27,Yn 7:3-6,Yn 4:1-42,Yn 17:1-5,Efe 5:15-16,Yn 2:1-4,-NKJV)
Wajasiliamali wa kondomu kama babu yangu Karugendo ni mfano mzuri wa watu wanaopotosha umma kwa kusema eti Mungu ameasisi Kondomu,nasisitiza NI UPOTOSHAJI MKUBWA JAMANI TUSIKAE KIMYA!
Katika makala zangu za toleo 800 na 807 nilisema lengo la kitubio ni kurudisha urafiki uliopotea kati ya binadamu na Mungu wake na nikasema maungamo ya kweli ni yale yanayoendana na urekebishaji wa tabia,pia nikasisitiza kama mtu atarudia dhambi eti kisa kuna Mungu atamuondolea dhambi huyo atakuwa anamjaribu bwana Mungu wake!
Hebu ngoja tuangalie “philosophy” za kondomu,kimsingi kondomu inachochea ngono! Labda utaniuliza kivipi,pakiti za kondomu tulizo nazo madukani zina picha za “ponografia” hii inachochea ngono na inakwenda kinyume kabisa na sera ya serikali ya kuzuia picha za ngono. Pili kondomu zinafanya suala la kuacha kufanya ngono lisiwepo,kwa sababu kondomu inahubiriwa sana kuliko njia nyingine!
Mathalani kondomu zinawekwa “betri” hii itamfanya mtu ajizuie kufanya ngono kweli? Nyingine zinapewa majina ya kuonyesha umwamba katika kufanya ngono mfano kondomu inaitwa DUME!
Si-hivyo tu bali kondomu zinaharibu urafiki kati ya mtu na mtu,zinaondoa heshima ya tendo la ndoa,linaharibu maadili,na mengineyo mengi.
Pili imani zetu zinatuambia TUSIZINI lakini wajasiriamali wa kondomu wanasema TUZINI! Kwa kutumia silaha! Lakini wanashindwa kujibu swali Je kama tukitumia kondomu dhambi hatutapata?
Karugendo pia ameshindwa kujibu swali langu kuhusu kutokufanya ngono nilimuuliza ni ugonjwa gani mtu ataupata kama akikaa mda mrefu bila kufanya ngono?
Mpaka sasa hakuna mwanasayansi yeyote aliyehakikisha kama kondomu inazuia ukimwi 100%,labla mimba!
Tusidanganyike kondomu sio silaha! Ngono ina nguvu kuliko kondomu! Kuna tofauti kati ya kutumia silaha na kushika silaha! Na wataalamu wanatuambia akili ya binadamu kabla na baada ya kushika silaha ni tofauti! Hivyo silaha inaishia kukuua wewe mwenyewe! Silaha inareta kiburi cha muda tu.
Takwimu za NACP za October 2005 zinaonyesha maabukizi ya ukimwi yanaongezeka maradufu kwa mikoa ya Mbeya,Dar,Tanga na Kagera! pamoja na kutumika kwa kondomu!
Mwandishi katika makala iliyopita anasema “Si kweli kwamba mimi nimenunuliwa kuandika juu ya kondomu.Si kweli kabisa maana vinginevyo maisha yangu yangekuwa ya juu sana.hizo pesa zingeonekana tu “
Haya ni maneno mazito kwa mtu kama huyu! Lakini najiuliza mbona mimi sikumtuhumu wala kuandika juu ya yeye kununuliwa kuandika juu ya kondomu!
Mwandishi anaonyesha kujishuku na hapa kunakitu! haiwezekana akaanza kutoa hoja kama hizi! Mathalani huwezi ukapita kariakoo halafu mtu akaanza tu kusema “mimi sio mwizi! Mimi si mwizi” huyo atakuwa na lake jambo! Karugendo vipi?
Inawezekana Karugendo anahudhuria sana vijisemina na viwarsha kuhusu Matumizi ya Kondomu na hii inawaafanya watu kuhisi babu kanunuliwa kuandika kuhusu kondomu sasa aache afanye vitu vingine vipadiem hivi vitamponza!
Ukimwi na ngono haviwezi kuisha kama tutakazania kondomu! Ni jukumu letu kurudisha heshima ya tendo la ndoa kwani ni tendo takatifu.
Subiri na Tosheka naye ni ujumbe usiofaa kubezwa,Karugendo yampasa aache vionjo! Na aufuate UKWELI!
Ndimi
KILLIAN E. NANGO
P.O.BOX 9192
DAR ES SALAAM
Emaili:Killijunior@yahoo.com
“Mimi ni mwanafunzi wa mwaka wa PILI,taaluma ya Uhasibu katika Chuo cha usimamizi wa Fedha IFM-Dar Es Salaam.Msomaji makini wa Tanzania Daima Jumapili,na pia ni Mwanaharakati wa YUNA na TYVA”
Monday, March 19, 2007
Ukimwi na Kondomu
WANAOTUFUNDISHA KUTUMIA KONDOMU, WANATUFUNDISHA KUUA!
Mjadala juu ya matumizi ya kondomu umepamba moto na tumeshuhudia wajasiriamali wa kondomu wakiongezeka, aina za kondomu zikiongezeka tunaambiwa kuna kondomu zenye betri (Vibrating kondoms), kondomu zenye harufu mbalimbali! mfano harufu ya chungwa, embe, na nyinginezo nyingi haya ni maajabu ya Mussa!
Katika makala zilizopita za gazeti hili tumeshuhudia watu wanaotetea kondomu wakijenga hoja zisizo na ukweli wowote na kubaki wakipotosha umma! Hii ni hatari kwani upotofu unasambaa kama ilivyo kwa maambikizi ya ukimwi!
Kabla ya kuanza ya kutoa hoja labda tuangalie ni wapi ndugu zetu wamepotoka!
Mwanafalsafa wa siku nyingi Permanides anatuasa juu ya ukweli anasema watu wanachanganya kati ya ukweli kadri unavyojitokeza kwao-relative truth na ukweli halisi-objective truth anasema ni vizuri kuangalia kitu kama kilivyo na si-vinginevyo!, na hii ilimfanya mwanafalsafa Plato kuugawa ulimwengu katika makundi mawili,yaani ulimwengu wa busara na akili-intelligible world na ulimwengu wa mwonekano-sensible world na kadiri ya Plato wale wenye busara na fikara sahii wapo kwenye ulimwengu wa ukweli na wale wenye vionjo wapo kwenye ulimwengu wa maoni/maono!
Kwa hiyo wale wote wanaosema wanatoa maoni yao wapo kwenye ulimwengu wao wa VIONJO!
Labda tuangalie ukweli na uhalisia wa kondomu,Mosi azma ya awali ya kutengeneza kondomu haikuwa kuzuia ukimwi!
Pili mpaka sasa hakuna uthibitisho wowote uliotolewa na mwanasayansi ama taasisi yoyote kuhusu uwezo wa kondomu kuzuia ukimwi kwa 100%.
Tatu kama vitabu vyetu vitakatifu vinatuambia tusizini na kondomu inatuambia tuzini kwa kutumia silaha huku ni kuhalisha dhambi!
Nne falsafa ya kondomu kama inavyoendeshwa na wajasiriamali wa kondomu ni ya mauaji na kimsingi kondomu inafanya kazi kubwa mbili,moja kondomu inawasawishi watu wafanye ngono mfano picha nyingi sana zinazowekwa kwenye pakiti ya kondomu ni zile za ponografia na mengine niliyoyaeleza hapo juu ni wazi yanachochea ngono na tukumbuke sehemu wanazouza bidhaa hii wanaingia watu wa rika zote watoto,vijana na wazee kwa hiyo kuwaoshesha watoto ,vijana na wengine picha hizi ni kuwashawishi wafanye ngono na hili ni kinyume na sera za SERIKALI! Pili kupoteza pesa nyingi katika matangazo yanayosawishi matumizi ya kondomu na si-kuacha kufanya ngono hii ni dalili ya mauaji maana yake tunawashawishi watu waanze na C badala ya A au B.
Mfano Watu wengine wamefikia mpaka hatua za kubeza kampeni za SUBIRI AU TOSHEKA NAYE na wengine kuhusisha kondomu na kitubio hawa ni wauwaji wakubwa!
Na cha kushangaza utakuta watu hao labda walikuwa ni viongozi wa dini kwa miaka mingi iliyopita.
Lakini watu wanapata mashaka na watu hawa mosi kwa kadri ya taratibu za dini zao tunaambiwa watu hawa wanauishi useja je watu hawa waliishi maagizo haya? Kama waliishi maagizo haya je mbona wanawafundisha watu watumie kondomu? Na kama walishindwa kwa nini wanawashawishi watu wafuate maanguko yao?
Ukiangalia kwa makini maswali hayo utagundua watu hao utagundua hawana tofauti na wale aliowazungumzia mwanafalasafa Permanides na Plato yaani watu wa vionjo!
Lakini pili watu hao wanaolingalisha kondomu na kitubio utagundua kuwa wameshindwa kuelewa zana ya “mkosefu kusamehewa na aliyekosewa kusamehe” hii ni maana halisi ya KITUBIO kwa maana kitubio kinalenga katika kurudisha mahusiano yaliyopotea,lakini twaweza kusema kuwa watu hawa si-watu wanaowasamehe wenzao wala wao hawapedi kusamehewa na mara nyingi watu hawa huwa viburi wa upatanisho!
Lakini kundi lingine ni hawa wananchi wa kawaida ambao wao wamekuwa wahanga wa tatizo hili,kimsingi hawa wanapata wakati mgumu sana kwani wakati serikali ikiubili juu ya matumizi ya kondomu taasisi za dini zinahubiri juu ya maagizo ya kuacha kuzini na kutotumia kondomu!
Wanaotumia kondomu kwa maana ya kushindwa kujizuia kufanya ngono wameshindwa pia kufuata maagizo ya muumba wao.
Ukiangalia uumbaji wa dunia utaona mungu aliumbwa vitu vyote na na baadaye akasema na sasa tumuumbe mtawala wa hivi vyote wanyama, ndege, mimea, ardhi nk soma Mwa. 1:26-28 “Mungu akasema na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu, wakatawale samaki wa baharini na ndege wa angani na wanyama na nchi yote pia na kila kitambaacho juu ya nchi.Mungu akaumba mtu kwa mfano wake kwa mfano wa Mungu alimwumba mwanaume na mwanamke aliwaumba.Mungu akawabariki, mungu akawaambia zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha, mkawatawale samaki wa wa baharini na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi”
Maneno tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu, mwanaume, mwanamke, zaeni, ni maneno yanahitaji tafakari ya kina na utagundua binadamu kapewa mamlaka ya kutawala yote hata uzinzi!
Mazingira ya binadamu wa kwanza yaani Adamu na Eva ni yaleyale mfano wakati wale waliambiwa wasile matunda ya MTI WA UZIMA Mwa.2:15-17 sisi leo tunambiwa TUSIZINI na tumeshuhudia kwenye maandiko matakatifu madhara ya kukiuka maadili.
Matatizo mengi anayoyapata binadamu wa leo UKIMWI, RUSHWA, UMASIKINI, UHALIFU, ni matokeo ya kukiuka maadilI matakatifu.
Uongo juu ya uwezo wa kondomu kuzuia maambukizo ya ukimwi unafichuliwa katika taarifa za NACP, TACAIDS, mfano pamoja na kuongezeka kwa usambazaji na matumizi ya kondomu bado maambukizi yanaongezeka!
Binafsi naona kufundisha watu kutumia kondomu ni sawa tu na kuwafundisha watu namwa ya kuua! Mfano wanaofanya ngono wakiwa na virusi vya ukimwi kwa kutumia kondomu ni kuwafundisha watu kuua!!
Ni nani kwenye tendo la ndoa ata chukua kondomu ingine ili-hali ile aliyoivaa imetoboka au imevuka? Utajuaje kama kondomu imetoboka wakati wewe upo kwenye mshindo? Huku si kuwafundisha watu waue?
Kusema kondomu ni silaha ni kutuongopea! Na ni ubabaishaji mkubwa! Watu wananunua kondomu lakini pindi wanapoona tupu za wenzi wao kondomu ina-wekwa pembeni na watu wanaanza kufanza tendo la ndoa! Mwishoe wanaambukizana ukimwi!
Wataalamu wa saikolojia wasema maumbo ya binadamu yana nguvu kuliko kondomu na tendo la ngono lina nguvu kuliko kondomu hivyo utagundua kondomu si silaha bali UPOTOSHAJI TU!
Kamwe hatuwezi kutetea uhai,kuwa wema,kutenda haki, kumheshimu mungu kwa kutumia kondomu
Suala la kutotumia kondomu ama kuacha kufanya ngono/kuwa mwaminifu kwa mwenza wako kwa wale waliooa haliitaji MAJADILIANO/UTAMADUNISHO!
Hatuwezi kuheshimu uhai wa mtu kwa kuacha maadili ya Mungu yateketee! Tusiipake dhambi manukato dhambi ni dhambi tu! Kondomu haina uwezo wa kubadilisha dhambi kuwa tendo takatifu haiwezekani!
Kama tunataka kuheshimu uhai tuanze kuhubiri juu ya kuacha kufanya ngono kwa wale ambao hawajaoa kwani hakuna ugonjwa wowote unaosabibishwa na kutokufanya ngono! Pili tuhubiri juu ya uaminifu kwa wale wenye ndoa zao! Tatu tuhubiri juu ya kuheshimu maadili ya dini zetu.
Tuache ujasiriamali wa kondomu tutafute bidhaa nyingine za kuuza si kondomu haifai kuuzwa wala haiuziki!
Tukumbuke ya kuwa mafundisho ya vitabu vitakatifu yanasema TUSIUE wala TUSIZINI.
Na usanii wa Kufundisha watu kutumia kondomu kwa kigezo cha kuzuia ukimwi ni kuwafundisha watu kuua!
Ndimi
KILLIAN E. NANGO
P.O.BOX 9192
DAR ES SALAAM
Emaili:Killijunior@yahoo.com
“Mimi ni mwanafunzi wa mwaka wa PILI,taaluma ya Uhasibu katika Chuo cha usimamizi wa Fedha IFM-Dar Es Salaam.Msomaji makini wa Tanzania Daima Jumapili,na pia ni Mwanaharakati wa YUNA na TYVA”
Mjadala juu ya matumizi ya kondomu umepamba moto na tumeshuhudia wajasiriamali wa kondomu wakiongezeka, aina za kondomu zikiongezeka tunaambiwa kuna kondomu zenye betri (Vibrating kondoms), kondomu zenye harufu mbalimbali! mfano harufu ya chungwa, embe, na nyinginezo nyingi haya ni maajabu ya Mussa!
Katika makala zilizopita za gazeti hili tumeshuhudia watu wanaotetea kondomu wakijenga hoja zisizo na ukweli wowote na kubaki wakipotosha umma! Hii ni hatari kwani upotofu unasambaa kama ilivyo kwa maambikizi ya ukimwi!
Kabla ya kuanza ya kutoa hoja labda tuangalie ni wapi ndugu zetu wamepotoka!
Mwanafalsafa wa siku nyingi Permanides anatuasa juu ya ukweli anasema watu wanachanganya kati ya ukweli kadri unavyojitokeza kwao-relative truth na ukweli halisi-objective truth anasema ni vizuri kuangalia kitu kama kilivyo na si-vinginevyo!, na hii ilimfanya mwanafalsafa Plato kuugawa ulimwengu katika makundi mawili,yaani ulimwengu wa busara na akili-intelligible world na ulimwengu wa mwonekano-sensible world na kadiri ya Plato wale wenye busara na fikara sahii wapo kwenye ulimwengu wa ukweli na wale wenye vionjo wapo kwenye ulimwengu wa maoni/maono!
Kwa hiyo wale wote wanaosema wanatoa maoni yao wapo kwenye ulimwengu wao wa VIONJO!
Labda tuangalie ukweli na uhalisia wa kondomu,Mosi azma ya awali ya kutengeneza kondomu haikuwa kuzuia ukimwi!
Pili mpaka sasa hakuna uthibitisho wowote uliotolewa na mwanasayansi ama taasisi yoyote kuhusu uwezo wa kondomu kuzuia ukimwi kwa 100%.
Tatu kama vitabu vyetu vitakatifu vinatuambia tusizini na kondomu inatuambia tuzini kwa kutumia silaha huku ni kuhalisha dhambi!
Nne falsafa ya kondomu kama inavyoendeshwa na wajasiriamali wa kondomu ni ya mauaji na kimsingi kondomu inafanya kazi kubwa mbili,moja kondomu inawasawishi watu wafanye ngono mfano picha nyingi sana zinazowekwa kwenye pakiti ya kondomu ni zile za ponografia na mengine niliyoyaeleza hapo juu ni wazi yanachochea ngono na tukumbuke sehemu wanazouza bidhaa hii wanaingia watu wa rika zote watoto,vijana na wazee kwa hiyo kuwaoshesha watoto ,vijana na wengine picha hizi ni kuwashawishi wafanye ngono na hili ni kinyume na sera za SERIKALI! Pili kupoteza pesa nyingi katika matangazo yanayosawishi matumizi ya kondomu na si-kuacha kufanya ngono hii ni dalili ya mauaji maana yake tunawashawishi watu waanze na C badala ya A au B.
Mfano Watu wengine wamefikia mpaka hatua za kubeza kampeni za SUBIRI AU TOSHEKA NAYE na wengine kuhusisha kondomu na kitubio hawa ni wauwaji wakubwa!
Na cha kushangaza utakuta watu hao labda walikuwa ni viongozi wa dini kwa miaka mingi iliyopita.
Lakini watu wanapata mashaka na watu hawa mosi kwa kadri ya taratibu za dini zao tunaambiwa watu hawa wanauishi useja je watu hawa waliishi maagizo haya? Kama waliishi maagizo haya je mbona wanawafundisha watu watumie kondomu? Na kama walishindwa kwa nini wanawashawishi watu wafuate maanguko yao?
Ukiangalia kwa makini maswali hayo utagundua watu hao utagundua hawana tofauti na wale aliowazungumzia mwanafalasafa Permanides na Plato yaani watu wa vionjo!
Lakini pili watu hao wanaolingalisha kondomu na kitubio utagundua kuwa wameshindwa kuelewa zana ya “mkosefu kusamehewa na aliyekosewa kusamehe” hii ni maana halisi ya KITUBIO kwa maana kitubio kinalenga katika kurudisha mahusiano yaliyopotea,lakini twaweza kusema kuwa watu hawa si-watu wanaowasamehe wenzao wala wao hawapedi kusamehewa na mara nyingi watu hawa huwa viburi wa upatanisho!
Lakini kundi lingine ni hawa wananchi wa kawaida ambao wao wamekuwa wahanga wa tatizo hili,kimsingi hawa wanapata wakati mgumu sana kwani wakati serikali ikiubili juu ya matumizi ya kondomu taasisi za dini zinahubiri juu ya maagizo ya kuacha kuzini na kutotumia kondomu!
Wanaotumia kondomu kwa maana ya kushindwa kujizuia kufanya ngono wameshindwa pia kufuata maagizo ya muumba wao.
Ukiangalia uumbaji wa dunia utaona mungu aliumbwa vitu vyote na na baadaye akasema na sasa tumuumbe mtawala wa hivi vyote wanyama, ndege, mimea, ardhi nk soma Mwa. 1:26-28 “Mungu akasema na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu, wakatawale samaki wa baharini na ndege wa angani na wanyama na nchi yote pia na kila kitambaacho juu ya nchi.Mungu akaumba mtu kwa mfano wake kwa mfano wa Mungu alimwumba mwanaume na mwanamke aliwaumba.Mungu akawabariki, mungu akawaambia zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha, mkawatawale samaki wa wa baharini na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi”
Maneno tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu, mwanaume, mwanamke, zaeni, ni maneno yanahitaji tafakari ya kina na utagundua binadamu kapewa mamlaka ya kutawala yote hata uzinzi!
Mazingira ya binadamu wa kwanza yaani Adamu na Eva ni yaleyale mfano wakati wale waliambiwa wasile matunda ya MTI WA UZIMA Mwa.2:15-17 sisi leo tunambiwa TUSIZINI na tumeshuhudia kwenye maandiko matakatifu madhara ya kukiuka maadili.
Matatizo mengi anayoyapata binadamu wa leo UKIMWI, RUSHWA, UMASIKINI, UHALIFU, ni matokeo ya kukiuka maadilI matakatifu.
Uongo juu ya uwezo wa kondomu kuzuia maambukizo ya ukimwi unafichuliwa katika taarifa za NACP, TACAIDS, mfano pamoja na kuongezeka kwa usambazaji na matumizi ya kondomu bado maambukizi yanaongezeka!
Binafsi naona kufundisha watu kutumia kondomu ni sawa tu na kuwafundisha watu namwa ya kuua! Mfano wanaofanya ngono wakiwa na virusi vya ukimwi kwa kutumia kondomu ni kuwafundisha watu kuua!!
Ni nani kwenye tendo la ndoa ata chukua kondomu ingine ili-hali ile aliyoivaa imetoboka au imevuka? Utajuaje kama kondomu imetoboka wakati wewe upo kwenye mshindo? Huku si kuwafundisha watu waue?
Kusema kondomu ni silaha ni kutuongopea! Na ni ubabaishaji mkubwa! Watu wananunua kondomu lakini pindi wanapoona tupu za wenzi wao kondomu ina-wekwa pembeni na watu wanaanza kufanza tendo la ndoa! Mwishoe wanaambukizana ukimwi!
Wataalamu wa saikolojia wasema maumbo ya binadamu yana nguvu kuliko kondomu na tendo la ngono lina nguvu kuliko kondomu hivyo utagundua kondomu si silaha bali UPOTOSHAJI TU!
Kamwe hatuwezi kutetea uhai,kuwa wema,kutenda haki, kumheshimu mungu kwa kutumia kondomu
Suala la kutotumia kondomu ama kuacha kufanya ngono/kuwa mwaminifu kwa mwenza wako kwa wale waliooa haliitaji MAJADILIANO/UTAMADUNISHO!
Hatuwezi kuheshimu uhai wa mtu kwa kuacha maadili ya Mungu yateketee! Tusiipake dhambi manukato dhambi ni dhambi tu! Kondomu haina uwezo wa kubadilisha dhambi kuwa tendo takatifu haiwezekani!
Kama tunataka kuheshimu uhai tuanze kuhubiri juu ya kuacha kufanya ngono kwa wale ambao hawajaoa kwani hakuna ugonjwa wowote unaosabibishwa na kutokufanya ngono! Pili tuhubiri juu ya uaminifu kwa wale wenye ndoa zao! Tatu tuhubiri juu ya kuheshimu maadili ya dini zetu.
Tuache ujasiriamali wa kondomu tutafute bidhaa nyingine za kuuza si kondomu haifai kuuzwa wala haiuziki!
Tukumbuke ya kuwa mafundisho ya vitabu vitakatifu yanasema TUSIUE wala TUSIZINI.
Na usanii wa Kufundisha watu kutumia kondomu kwa kigezo cha kuzuia ukimwi ni kuwafundisha watu kuua!
Ndimi
KILLIAN E. NANGO
P.O.BOX 9192
DAR ES SALAAM
Emaili:Killijunior@yahoo.com
“Mimi ni mwanafunzi wa mwaka wa PILI,taaluma ya Uhasibu katika Chuo cha usimamizi wa Fedha IFM-Dar Es Salaam.Msomaji makini wa Tanzania Daima Jumapili,na pia ni Mwanaharakati wa YUNA na TYVA”
Subscribe to:
Comments (Atom)